5. Wapate kukulinda na malaya,Na mgeni akubembelezaye kwa maneno yake.
6. Maana katika dirisha la nyumba yanguNalichungulia katika shubaka yake;
7. Nikaona katikati ya wajinga,Nikamtambua miongoni mwa vijana,Kijana mmoja asiyekuwa na akili,
8. Akipita njiani karibu na pembe yake,Akiishika njia iendayo nyumbani kwake,
9. Wakati wa magharibi, wakati wa jioni,Usiku wa manane, gizani.
10. Na tazama, mwanamke akamkuta,Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;
11. Ana kelele, na ukaidi;Miguu yake haikai nyumbani mwake.