22. Huyo akafuatana naye mara hiyo,Kama vile ng’ombe aendavyo machinjoni;Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu;
23. Hata mshale umchome maini;Kama ndege aendaye haraka mtegoni;Wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake.
24. Basi, wanangu, nisikilizeni sasa,Mkayaangalie maneno ya kinywa changu.
25. Moyo wako usizielekee njia zake,Wala usipotee katika mapito yake.