Mit. 7:15-25 Swahili Union Version (SUV)

15. Ndiyo maana nikatoka nikulaki,Nikutafute uso wako kwa bidii, nami nimekuona.

16. Nimetandika kitanda changu, magodoro mazuri,Kwa matandiko ya Kimisri yenye mistari.

17. Nimetia kitanda changu manukato,Manemane na udi na mdalasini.

18. Haya, na tushibe upendo hata asubuhi,Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba.

19. Maana mume wangu hayumo nyumbani,Amekwenda safari ya mbali;

20. Amechukua mfuko wa fedha mkononi;Atarudi wakati wa mwezi mpevu.

21. Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi,Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda.

22. Huyo akafuatana naye mara hiyo,Kama vile ng’ombe aendavyo machinjoni;Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu;

23. Hata mshale umchome maini;Kama ndege aendaye haraka mtegoni;Wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake.

24. Basi, wanangu, nisikilizeni sasa,Mkayaangalie maneno ya kinywa changu.

25. Moyo wako usizielekee njia zake,Wala usipotee katika mapito yake.

Mit. 7