10. Na tazama, mwanamke akamkuta,Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;
11. Ana kelele, na ukaidi;Miguu yake haikai nyumbani mwake.
12. Mara yu katika njia kuu, mara viwanjani,Naye huotea kwenye pembe za kila njia.
13. Basi akamshika, akambusu,Akamwambia kwa uso usio na haya,
14. Kwangu ziko sadaka za amani;Leo hivi nimeziondoa nadhiri zangu;
15. Ndiyo maana nikatoka nikulaki,Nikutafute uso wako kwa bidii, nami nimekuona.
16. Nimetandika kitanda changu, magodoro mazuri,Kwa matandiko ya Kimisri yenye mistari.
17. Nimetia kitanda changu manukato,Manemane na udi na mdalasini.
18. Haya, na tushibe upendo hata asubuhi,Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba.
19. Maana mume wangu hayumo nyumbani,Amekwenda safari ya mbali;
20. Amechukua mfuko wa fedha mkononi;Atarudi wakati wa mwezi mpevu.
21. Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi,Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda.