1. Mwanangu, yashike maneno yangu,Na kuziweka amri zangu akiba kwako.
2. Uzishike amri zangu ukaishi,Na sheria yangu kama mboni ya jicho lako.
3. Zifunge katika vidole vyako;Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.
4. Mwambie hekima, Wewe ndiwe umbu langu;Mwite ufahamu jamaa yako mwanamke.
5. Wapate kukulinda na malaya,Na mgeni akubembelezaye kwa maneno yake.
6. Maana katika dirisha la nyumba yanguNalichungulia katika shubaka yake;