Mit. 7:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Mwanangu, yashike maneno yangu,Na kuziweka amri zangu akiba kwako.

2. Uzishike amri zangu ukaishi,Na sheria yangu kama mboni ya jicho lako.

3. Zifunge katika vidole vyako;Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.

4. Mwambie hekima, Wewe ndiwe umbu langu;Mwite ufahamu jamaa yako mwanamke.

5. Wapate kukulinda na malaya,Na mgeni akubembelezaye kwa maneno yake.

6. Maana katika dirisha la nyumba yanguNalichungulia katika shubaka yake;

Mit. 7