8. Lakini hujiwekea akiba ya chakula wakati wa jua;Hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
9. Ewe mvivu, utalala hata lini?Utaondoka lini katika usingizi wako?
10. Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,Bado kukunja mikono upate usingizi!
11. Hivyo umaskini wako huja kama mnyang’anyi,Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.
12. Mtu asiyefaa kitu, mtu wa uovu;Huenda njiani mwenye kinywa cha upotofu.
13. Hukonyeza kwa macho, hunena kwa miguu,Huwaashiria watu kwa vidole vyake.