Mit. 6:28-34 Swahili Union Version (SUV)

28. Je! Mtu aweza kukanyaga makaa ya moto,Na nyayo zake zisiungue?

29. Ndivyo alivyo aingiaye kwa mke wa jirani yake;Kila mtu amgusaye huyo atakuwa na hatia.

30. Watu hawamdharau mwivi,Akiiba ili kujishibisha, iwapo aona njaa;

31. Lakini akipatikana, atalipa mara saba;Atatoa mali yote ya nyumba yake.

32. Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa;Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.

33. Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima;Wala fedheha yake haitafutika.

34. Maana wivu ni ghadhabu ya mtu;Wala hatahurumia siku ya kujilipiza kisasi.

Mit. 6