8. Itenge njia yako mbali naye,Wala usiukaribie mlango wa nyumba yake.
9. Usije ukawapa wengine heshima yako,Na wakorofi miaka yako;
10. Wageni wasije wakashiba nguvu zako;Kazi zako zikawa ndani ya nyumba ya mgeni;
11. Nawe ukaziombolea siku zako za mwisho,Nyama yako na mwili wako utakapoangamia;
12. Ukasema, Jinsi nilivyochukia maonyo,Na moyo wangu ukadharau kukemewa;
13. Wala sikuisikia sauti ya waalimu wangu,Wala sikuwategea sikio langu walionifundisha!
14. Nalikuwa karibu na kuingia katika maovu yote,Katikati ya mkutano na kusanyiko.