Mit. 5:8-14 Swahili Union Version (SUV)

8. Itenge njia yako mbali naye,Wala usiukaribie mlango wa nyumba yake.

9. Usije ukawapa wengine heshima yako,Na wakorofi miaka yako;

10. Wageni wasije wakashiba nguvu zako;Kazi zako zikawa ndani ya nyumba ya mgeni;

11. Nawe ukaziombolea siku zako za mwisho,Nyama yako na mwili wako utakapoangamia;

12. Ukasema, Jinsi nilivyochukia maonyo,Na moyo wangu ukadharau kukemewa;

13. Wala sikuisikia sauti ya waalimu wangu,Wala sikuwategea sikio langu walionifundisha!

14. Nalikuwa karibu na kuingia katika maovu yote,Katikati ya mkutano na kusanyiko.

Mit. 5