Mit. 5:19-22 Swahili Union Version (SUV)

19. Ni ayala apendaye na paa apendezaye;Maziwa yake yakutoshe sikuzote;Na kwa upendo wake ushangilie daima.

20. Mwanangu! Mbona unashangilia malaya,Na kukikumbatia kifua cha mgeni?

21. Kwa maana njia za mwanadamu zi mbele za macho ya BWANA,Na mienendo yake yote huitafakari.

22. Maovu yake yeye yatampata mdhalimu,Naye atashikwa kwa kamba za dhambi zake.

Mit. 5