Mit. 5:1-10 Swahili Union Version (SUV)

1. Mwanangu, sikiliza hekima yangu;Tega sikio lako, mzisikie akili zangu;

2. Upate kuilinda busara,Na midomo yako iyahifadhi maarifa.

3. Maana midomo ya malaya hudondoza asali,Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta;

4. Lakini mwisho wake ni mchungu kuliko pakanga;Ni mkali kama upanga wa makali kuwili.

5. Miguu yake inatelemkia mauti;Hatua zake zinashikamana na kuzimu;

6. Hata asiweze kuiona njia sawa ya uzima;Njia zake ni za kutanga-tanga wala hana habari.

7. Basi, wanangu, nisikilizeni sasa,Wala msiache maneno ya kinywa changu.

8. Itenge njia yako mbali naye,Wala usiukaribie mlango wa nyumba yake.

9. Usije ukawapa wengine heshima yako,Na wakorofi miaka yako;

10. Wageni wasije wakashiba nguvu zako;Kazi zako zikawa ndani ya nyumba ya mgeni;

Mit. 5