Mit. 4:6-14 Swahili Union Version (SUV)

6. Usimwache, naye atakuhifadhi;Umpende, naye atakulinda.

7. Bora hekima, basi jipatie hekima;Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.

8. Umtukuze, naye atakukuza;Atakupatia heshima, ukimkumbatia.

9. Atakupa neema kuwa kilemba kichwani;Na kukukirimia taji ya uzuri.

10. Mwanangu, sikiliza, na kuzipokea kauli zangu;Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi.

11. Nimekufundisha katika njia ya hekima;Nimekuongoza katika mapito ya unyofu.

12. Uendapo, hatua zako hazitadhiikika,Wala ukipiga mbio hutajikwaa.

13. Mkamate sana elimu, usimwache aende zake;Mshike, maana yeye ni uzima wako.

14. Usiingie katika njia ya waovu,Wala usitembee katika njia ya wabaya.

Mit. 4