Mit. 4:1-8 Swahili Union Version (SUV)

1. Wanangu, yasikilizeni mausia ya baba yenu,Tegeni masikio mpate kujua ufahamu.

2. Kwa kuwa nawapa mafundisho mazuri;Msiiache sheria yangu.

3. Maana nalikuwa mwana kwa baba yangu,Mpole, mpenzi wa pekee wa mama yangu.

4. Naye akanifundisha, akaniambia,Moyo wako uyahifadhi maneno yangu;Shika amri zangu ukaishi.

5. Jipatie hekima, jipatie ufahamu; usiusahau;Wala usiyakatae maneno ya kinywa changu.

6. Usimwache, naye atakuhifadhi;Umpende, naye atakulinda.

7. Bora hekima, basi jipatie hekima;Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.

8. Umtukuze, naye atakukuza;Atakupatia heshima, ukimkumbatia.

Mit. 4