7. Mambo haya mawili nimekuomba;Usininyime [matatu] kabla sijafa.
8. Uniondolee ubatili na uongo;Usinipe umaskini wala utajiri;Unilishe chakula kilicho kadiri yangu.
9. Nisije nikashiba nikakukana,Nikasema, BWANA ni nani?Wala nisiwe maskini sana nikaiba,Na kulitaja bure jina la Mungu wangu.
10. Usimchongee mtumwa kwa bwana wake;Asije akakulaani, ukaonekana una hatia.
11. Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao;Wala hawambariki mama yao.
12. Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao wenyewe;Ambao hawakuoshwa uchafu wao.