5. Kila neno la Mungu limehakikishwa;Yeye ni ngao yao wamwaminio.
6. Usiongeze neno katika maneno yake;Asije akakulaumu, ukaonekana u mwongo.
7. Mambo haya mawili nimekuomba;Usininyime [matatu] kabla sijafa.
8. Uniondolee ubatili na uongo;Usinipe umaskini wala utajiri;Unilishe chakula kilicho kadiri yangu.
9. Nisije nikashiba nikakukana,Nikasema, BWANA ni nani?Wala nisiwe maskini sana nikaiba,Na kulitaja bure jina la Mungu wangu.
10. Usimchongee mtumwa kwa bwana wake;Asije akakulaani, ukaonekana una hatia.
11. Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao;Wala hawambariki mama yao.
12. Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao wenyewe;Ambao hawakuoshwa uchafu wao.
13. Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini!Na kope zao zimeinuka sana.
14. Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga;Na vigego vyao ni kama visu.Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu.
15. Mruba anao binti wawili,Waliao, Nipe! Nipe!Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe,Naam, vinne visivyosema, Basi!