Mit. 30:5-15 Swahili Union Version (SUV)

5. Kila neno la Mungu limehakikishwa;Yeye ni ngao yao wamwaminio.

6. Usiongeze neno katika maneno yake;Asije akakulaumu, ukaonekana u mwongo.

7. Mambo haya mawili nimekuomba;Usininyime [matatu] kabla sijafa.

8. Uniondolee ubatili na uongo;Usinipe umaskini wala utajiri;Unilishe chakula kilicho kadiri yangu.

9. Nisije nikashiba nikakukana,Nikasema, BWANA ni nani?Wala nisiwe maskini sana nikaiba,Na kulitaja bure jina la Mungu wangu.

10. Usimchongee mtumwa kwa bwana wake;Asije akakulaani, ukaonekana una hatia.

11. Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao;Wala hawambariki mama yao.

12. Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao wenyewe;Ambao hawakuoshwa uchafu wao.

13. Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini!Na kope zao zimeinuka sana.

14. Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga;Na vigego vyao ni kama visu.Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu.

15. Mruba anao binti wawili,Waliao, Nipe! Nipe!Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe,Naam, vinne visivyosema, Basi!

Mit. 30