Mit. 30:22-28 Swahili Union Version (SUV)

22. Mtumwa apatapo kuwa mfalme;Mpumbavu ashibapo chakula;

23. Mwanamke mwenye kuchukiza aolewapo;Na mjakazi aliye mrithi wa bibi yake.

24. Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo;Lakini vina akili nyingi sana.

25. Chungu ni watu wasio na nguvu;Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.

26. Wibari ni watu dhaifu;Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.

27. Nzige hawana mfalme;Lakini huenda wote pamoja vikosi vikosi.

28. Mjusi hushika kwa mikono yake;Lakini yumo majumbani mwa wafalme.

Mit. 30