Mit. 30:21-30 Swahili Union Version (SUV)

21. Kwa ajili ya mambo matatu nchi hutetemeka,Naam, kwa ajili ya manne haiwezi kuvumilia.

22. Mtumwa apatapo kuwa mfalme;Mpumbavu ashibapo chakula;

23. Mwanamke mwenye kuchukiza aolewapo;Na mjakazi aliye mrithi wa bibi yake.

24. Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo;Lakini vina akili nyingi sana.

25. Chungu ni watu wasio na nguvu;Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.

26. Wibari ni watu dhaifu;Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.

27. Nzige hawana mfalme;Lakini huenda wote pamoja vikosi vikosi.

28. Mjusi hushika kwa mikono yake;Lakini yumo majumbani mwa wafalme.

29. Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza,Naam, wanne walio na mwendo mzuri.

30. Simba aliye hodari kupita wanyama wote;Wala hajiepushi na aliye yote;

Mit. 30