Mit. 30:17-31 Swahili Union Version (SUV)

17. Jicho la mtu amdhihakiye babaye,Na kudharau kumtii mamaye;Kunguru wa bondeni wataling’oa,Na vifaranga vya tai watalila.

18. Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu,Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.

19. Mwendo wa tai katika hewa;Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba;Mwendo wa merikebu katikati ya bahari;Na mwendo wa mtu pamoja na msichana.

20. Hivyo ndivyo mwendo wa mwanamke mzinifu;Hula, akapangusa kinywa chake,Akasema, Sikufanya uovu.

21. Kwa ajili ya mambo matatu nchi hutetemeka,Naam, kwa ajili ya manne haiwezi kuvumilia.

22. Mtumwa apatapo kuwa mfalme;Mpumbavu ashibapo chakula;

23. Mwanamke mwenye kuchukiza aolewapo;Na mjakazi aliye mrithi wa bibi yake.

24. Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo;Lakini vina akili nyingi sana.

25. Chungu ni watu wasio na nguvu;Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.

26. Wibari ni watu dhaifu;Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.

27. Nzige hawana mfalme;Lakini huenda wote pamoja vikosi vikosi.

28. Mjusi hushika kwa mikono yake;Lakini yumo majumbani mwa wafalme.

29. Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza,Naam, wanne walio na mwendo mzuri.

30. Simba aliye hodari kupita wanyama wote;Wala hajiepushi na aliye yote;

31. Jimbi aendaye tambo; na beberu;Na mfalme ambaye haasiki.

Mit. 30