17. Jicho la mtu amdhihakiye babaye,Na kudharau kumtii mamaye;Kunguru wa bondeni wataling’oa,Na vifaranga vya tai watalila.
18. Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu,Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.
19. Mwendo wa tai katika hewa;Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba;Mwendo wa merikebu katikati ya bahari;Na mwendo wa mtu pamoja na msichana.
20. Hivyo ndivyo mwendo wa mwanamke mzinifu;Hula, akapangusa kinywa chake,Akasema, Sikufanya uovu.
21. Kwa ajili ya mambo matatu nchi hutetemeka,Naam, kwa ajili ya manne haiwezi kuvumilia.
22. Mtumwa apatapo kuwa mfalme;Mpumbavu ashibapo chakula;
23. Mwanamke mwenye kuchukiza aolewapo;Na mjakazi aliye mrithi wa bibi yake.
24. Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo;Lakini vina akili nyingi sana.
25. Chungu ni watu wasio na nguvu;Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.
26. Wibari ni watu dhaifu;Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.
27. Nzige hawana mfalme;Lakini huenda wote pamoja vikosi vikosi.
28. Mjusi hushika kwa mikono yake;Lakini yumo majumbani mwa wafalme.
29. Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza,Naam, wanne walio na mwendo mzuri.
30. Simba aliye hodari kupita wanyama wote;Wala hajiepushi na aliye yote;
31. Jimbi aendaye tambo; na beberu;Na mfalme ambaye haasiki.