13. Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini!Na kope zao zimeinuka sana.
14. Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga;Na vigego vyao ni kama visu.Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu.
15. Mruba anao binti wawili,Waliao, Nipe! Nipe!Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe,Naam, vinne visivyosema, Basi!
16. Kuzimu; na tumbo lisilozaa;Nchi isiyoshiba maji; na moto usiosema, Basi!
17. Jicho la mtu amdhihakiye babaye,Na kudharau kumtii mamaye;Kunguru wa bondeni wataling’oa,Na vifaranga vya tai watalila.
18. Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu,Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.
19. Mwendo wa tai katika hewa;Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba;Mwendo wa merikebu katikati ya bahari;Na mwendo wa mtu pamoja na msichana.
20. Hivyo ndivyo mwendo wa mwanamke mzinifu;Hula, akapangusa kinywa chake,Akasema, Sikufanya uovu.
21. Kwa ajili ya mambo matatu nchi hutetemeka,Naam, kwa ajili ya manne haiwezi kuvumilia.
22. Mtumwa apatapo kuwa mfalme;Mpumbavu ashibapo chakula;
23. Mwanamke mwenye kuchukiza aolewapo;Na mjakazi aliye mrithi wa bibi yake.
24. Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo;Lakini vina akili nyingi sana.
25. Chungu ni watu wasio na nguvu;Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.