7. Usiwe mwenye hekima machoni pako;Mche BWANA, ukajiepushe na uovu.
8. Itakuwa afya mwilini pako,Na mafuta mifupani mwako.
9. Mheshimu BWANA kwa mali yako,Na kwa malimbuko ya mazao yako yote.
10. Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi,Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya.
11. Mwanangu, usidharau kuadhibiwa na BWANA,Wala usione ni taabu kurudiwa naye.
12. Kwa kuwa BWANA ampendaye humrudi,Kama vile baba mwanawe ampendezaye.