Mit. 3:18-22 Swahili Union Version (SUV)

18. Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana;Ana heri kila mtu ashikamanaye naye.

19. Kwa hekima BWANA aliiweka misingi ya nchi;Kwa akili zake akazifanya mbingu imara;

20. Kwa maarifa yake vilindi viligawanyika;Na mawingu yadondoza umande.

21. Mwanangu, yasiondoke haya machoni pako,Shika hekima kamili na busara.

22. Basi yatakuwa uzima kwa nafsi yako,Na neema shingoni mwako.

Mit. 3