18. Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana;Ana heri kila mtu ashikamanaye naye.
19. Kwa hekima BWANA aliiweka misingi ya nchi;Kwa akili zake akazifanya mbingu imara;
20. Kwa maarifa yake vilindi viligawanyika;Na mawingu yadondoza umande.
21. Mwanangu, yasiondoke haya machoni pako,Shika hekima kamili na busara.
22. Basi yatakuwa uzima kwa nafsi yako,Na neema shingoni mwako.