10. Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi,Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya.
11. Mwanangu, usidharau kuadhibiwa na BWANA,Wala usione ni taabu kurudiwa naye.
12. Kwa kuwa BWANA ampendaye humrudi,Kama vile baba mwanawe ampendezaye.
13. Heri mtu yule aonaye hekima,Na mtu yule apataye ufahamu.
14. Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha,Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi.