8. Watu wenye dharau huwasha mji moto;Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.
9. Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu;Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
10. Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu;Bali wenye haki humtunza nafsi yake.
11. Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote;Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.