Mit. 29:8-11 Swahili Union Version (SUV)

8. Watu wenye dharau huwasha mji moto;Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.

9. Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu;Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.

10. Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu;Bali wenye haki humtunza nafsi yake.

11. Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote;Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.

Mit. 29