7. Mwenye haki huyaangalia madai ya maskini;Bali mtu mbaya hana ufahamu hata ayajue.
8. Watu wenye dharau huwasha mji moto;Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.
9. Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu;Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
10. Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu;Bali wenye haki humtunza nafsi yake.
11. Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote;Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.
12. Mwenye kutawala akisikiliza uongo;Basi watumishi wake wote watakuwa waovu.
13. Maskini na mdhalimu hukutana pamoja;BWANA huwatia nuru macho yao wote wawili.
14. Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu;Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.
15. Fimbo na maonyo hutia hekima;Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.
16. Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka;Bali wenye haki watayatazama maanguko yao.
17. Mrudi mwanao naye atakustarehesha;Naam, atakufurahisha nafsi yako.
18. Pasipo maono, watu huacha kujizuia;Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.