Mit. 29:6-14 Swahili Union Version (SUV)

6. Kuna mtego katika kosa la mtu mbaya;Bali mwenye haki huimba na kufurahi.

7. Mwenye haki huyaangalia madai ya maskini;Bali mtu mbaya hana ufahamu hata ayajue.

8. Watu wenye dharau huwasha mji moto;Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.

9. Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu;Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.

10. Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu;Bali wenye haki humtunza nafsi yake.

11. Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote;Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.

12. Mwenye kutawala akisikiliza uongo;Basi watumishi wake wote watakuwa waovu.

13. Maskini na mdhalimu hukutana pamoja;BWANA huwatia nuru macho yao wote wawili.

14. Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu;Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.

Mit. 29