3. Apendaye hekima humfurahisha babaye;Bali ashikamanaye na makahaba hutapanya mali.
4. Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu;Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.
5. Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake,Hutandika wavu ili kuitega miguu yake.
6. Kuna mtego katika kosa la mtu mbaya;Bali mwenye haki huimba na kufurahi.
7. Mwenye haki huyaangalia madai ya maskini;Bali mtu mbaya hana ufahamu hata ayajue.
8. Watu wenye dharau huwasha mji moto;Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.
9. Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu;Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
10. Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu;Bali wenye haki humtunza nafsi yake.
11. Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote;Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.
12. Mwenye kutawala akisikiliza uongo;Basi watumishi wake wote watakuwa waovu.