Mit. 29:23-27 Swahili Union Version (SUV)

23. Kiburi cha mtu kitamshusha;Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.

24. Mshiriki wa mwivi huichukia nafsi yake mwenyewe;Asikia maapizo, wala hana neno.

25. Kuwaogopa wanadamu huleta mtego;Bali amtumainiye BWANA atakuwa salama.

26. Watu wengi hutafuta upendeleo wa mkuu;Bali hukumu ya kila mtu hutoka kwa BWANA

27. Mtu aliye dhalimu ni chukizo kwa wenye haki;Na mnyofu wa mwenendo ni chukizo kwa waovu.

Mit. 29