21. Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto,Mwisho wake atakuwa ni mwanawe.
22. Mtu wa hasira huchochea ugomvi;Na mtu mwenye ghadhabu huasi sana.
23. Kiburi cha mtu kitamshusha;Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.
24. Mshiriki wa mwivi huichukia nafsi yake mwenyewe;Asikia maapizo, wala hana neno.
25. Kuwaogopa wanadamu huleta mtego;Bali amtumainiye BWANA atakuwa salama.
26. Watu wengi hutafuta upendeleo wa mkuu;Bali hukumu ya kila mtu hutoka kwa BWANA
27. Mtu aliye dhalimu ni chukizo kwa wenye haki;Na mnyofu wa mwenendo ni chukizo kwa waovu.