Mit. 29:21-27 Swahili Union Version (SUV)

21. Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto,Mwisho wake atakuwa ni mwanawe.

22. Mtu wa hasira huchochea ugomvi;Na mtu mwenye ghadhabu huasi sana.

23. Kiburi cha mtu kitamshusha;Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.

24. Mshiriki wa mwivi huichukia nafsi yake mwenyewe;Asikia maapizo, wala hana neno.

25. Kuwaogopa wanadamu huleta mtego;Bali amtumainiye BWANA atakuwa salama.

26. Watu wengi hutafuta upendeleo wa mkuu;Bali hukumu ya kila mtu hutoka kwa BWANA

27. Mtu aliye dhalimu ni chukizo kwa wenye haki;Na mnyofu wa mwenendo ni chukizo kwa waovu.

Mit. 29