Mit. 29:2-6 Swahili Union Version (SUV)

2. Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi;Bali mwovu atawalapo, watu huugua.

3. Apendaye hekima humfurahisha babaye;Bali ashikamanaye na makahaba hutapanya mali.

4. Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu;Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.

5. Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake,Hutandika wavu ili kuitega miguu yake.

6. Kuna mtego katika kosa la mtu mbaya;Bali mwenye haki huimba na kufurahi.

Mit. 29