Mit. 29:14-21 Swahili Union Version (SUV)

14. Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu;Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.

15. Fimbo na maonyo hutia hekima;Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.

16. Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka;Bali wenye haki watayatazama maanguko yao.

17. Mrudi mwanao naye atakustarehesha;Naam, atakufurahisha nafsi yako.

18. Pasipo maono, watu huacha kujizuia;Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.

19. Haitoshi mtumwa kuonywa kwa maneno;Maana ajapoyafahamu hataitika.

20. Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno?Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.

21. Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto,Mwisho wake atakuwa ni mwanawe.

Mit. 29