14. Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu;Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.
15. Fimbo na maonyo hutia hekima;Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.
16. Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka;Bali wenye haki watayatazama maanguko yao.
17. Mrudi mwanao naye atakustarehesha;Naam, atakufurahisha nafsi yako.
18. Pasipo maono, watu huacha kujizuia;Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19. Haitoshi mtumwa kuonywa kwa maneno;Maana ajapoyafahamu hataitika.
20. Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno?Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.
21. Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto,Mwisho wake atakuwa ni mwanawe.