12. Mwenye kutawala akisikiliza uongo;Basi watumishi wake wote watakuwa waovu.
13. Maskini na mdhalimu hukutana pamoja;BWANA huwatia nuru macho yao wote wawili.
14. Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu;Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.
15. Fimbo na maonyo hutia hekima;Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.
16. Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka;Bali wenye haki watayatazama maanguko yao.
17. Mrudi mwanao naye atakustarehesha;Naam, atakufurahisha nafsi yako.
18. Pasipo maono, watu huacha kujizuia;Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19. Haitoshi mtumwa kuonywa kwa maneno;Maana ajapoyafahamu hataitika.
20. Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno?Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.
21. Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto,Mwisho wake atakuwa ni mwanawe.
22. Mtu wa hasira huchochea ugomvi;Na mtu mwenye ghadhabu huasi sana.
23. Kiburi cha mtu kitamshusha;Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.
24. Mshiriki wa mwivi huichukia nafsi yake mwenyewe;Asikia maapizo, wala hana neno.
25. Kuwaogopa wanadamu huleta mtego;Bali amtumainiye BWANA atakuwa salama.