Mit. 29:10-20 Swahili Union Version (SUV)

10. Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu;Bali wenye haki humtunza nafsi yake.

11. Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote;Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.

12. Mwenye kutawala akisikiliza uongo;Basi watumishi wake wote watakuwa waovu.

13. Maskini na mdhalimu hukutana pamoja;BWANA huwatia nuru macho yao wote wawili.

14. Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu;Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.

15. Fimbo na maonyo hutia hekima;Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.

16. Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka;Bali wenye haki watayatazama maanguko yao.

17. Mrudi mwanao naye atakustarehesha;Naam, atakufurahisha nafsi yako.

18. Pasipo maono, watu huacha kujizuia;Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.

19. Haitoshi mtumwa kuonywa kwa maneno;Maana ajapoyafahamu hataitika.

20. Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno?Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.

Mit. 29