1. Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo,Atavunjika ghafula, wala hapati dawa.
2. Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi;Bali mwovu atawalapo, watu huugua.
3. Apendaye hekima humfurahisha babaye;Bali ashikamanaye na makahaba hutapanya mali.
4. Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu;Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.
5. Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake,Hutandika wavu ili kuitega miguu yake.
6. Kuna mtego katika kosa la mtu mbaya;Bali mwenye haki huimba na kufurahi.
7. Mwenye haki huyaangalia madai ya maskini;Bali mtu mbaya hana ufahamu hata ayajue.
8. Watu wenye dharau huwasha mji moto;Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.
9. Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu;Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
10. Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu;Bali wenye haki humtunza nafsi yake.
11. Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote;Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.
12. Mwenye kutawala akisikiliza uongo;Basi watumishi wake wote watakuwa waovu.
13. Maskini na mdhalimu hukutana pamoja;BWANA huwatia nuru macho yao wote wawili.
14. Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu;Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.
15. Fimbo na maonyo hutia hekima;Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.
16. Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka;Bali wenye haki watayatazama maanguko yao.
17. Mrudi mwanao naye atakustarehesha;Naam, atakufurahisha nafsi yako.
18. Pasipo maono, watu huacha kujizuia;Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19. Haitoshi mtumwa kuonywa kwa maneno;Maana ajapoyafahamu hataitika.
20. Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno?Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.