Mit. 28:13-27 Swahili Union Version (SUV)

13. Afichaye dhambi zake hatafanikiwa;Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.

14. Mwanadamu mwenye kicho yu heri sikuzote;Bali mshupavu wa moyo ataangukia madhara.

15. Kama simba angurumaye, na dubu mwenye njaa;Ndivyo alivyo mtu mbaya awatawalaye maskini.

16. Mkuu aliyepungukiwa na akili huwaonea watu sana;Bali achukiaye kutamani ataongeza siku zake.

17. Aliyelemewa na damu ya mtuAtalikimbilia shimo; wala mtu asimzuie.

18. Aendaye kwa unyofu ataokolewa;Bali mkaidi wa njia zake ataanguka mara.

19. Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;Bali afuataye mambo ya upuzi atapata umaskini wa kumtosha.

20. Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.

21. Kupendelea watu si kwema;Wala mtu kuasi kwa ajili ya kipande cha mkate.

22. Mwenye husuda afanya haraka kuwa tajiri;Wala haufikiri uhitaji utakaomjilia.

23. Amkemeaye mwenzake hatimaye atapata kibali;Zaidi ya mtu ajipendekezaye kwa ulimi wake.

24. Aibaye mali ya babaye au mamaye, na kusema, Si kosa;Mwana huyo ni rafiki wa mtu mharibifu.

25. Mwenye nafsi ya kutamani huchochea fitina;Bali amtumainiye BWANA atawandishwa.

26. Mwenye kujitumainia moyo wake ni mjinga;Bali yeye aendaye kwa busara ataokolewa.

27. Mwenye kuwagawia maskini hatahitaji kitu;Bali afichaye macho yake atakuwa na laana nyingi.

Mit. 28