19. Kama uso ufananavyo na uso katika maji;Kadhalika moyo wa mtu na mwenzake.
20. Kuzimu na Uharibifu havishibi;Wala macho ya wanadamu hayashibi.
21. Kalibu ni kwa fedha, na tanuru kwa dhahabu;Na mtu hujaribiwa kwa sifa zake.
22. Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni pamoja na ngano;Upumbavu wake hautamtoka.
23. Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako;Na kuwaangalia sana ng’ombe zako.