Mit. 27:15-23 Swahili Union Version (SUV)

15. Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi,Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;

16. Atakaye kumzuia huyo huuzuia upepo;Na mkono wake wa kuume hukuta mafuta.

17. Chuma hunoa chuma;Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake.

18. Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;Naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.

19. Kama uso ufananavyo na uso katika maji;Kadhalika moyo wa mtu na mwenzake.

20. Kuzimu na Uharibifu havishibi;Wala macho ya wanadamu hayashibi.

21. Kalibu ni kwa fedha, na tanuru kwa dhahabu;Na mtu hujaribiwa kwa sifa zake.

22. Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni pamoja na ngano;Upumbavu wake hautamtoka.

23. Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako;Na kuwaangalia sana ng’ombe zako.

Mit. 27