Mit. 27:10-25 Swahili Union Version (SUV)

10. Usimwache rafiki yako mwenyewe, wala rafiki ya baba yako,Wala usiende nyumbani mwa ndugu yako siku ya msiba wako.Afadhali jirani aliye karibu kuliko ndugu aliye mbali.

11. Mwanangu, uwe na hekima na kunifurahisha moyo wangu;Ili nipate kumjibu anilaumuye.

12. Mwenye busara huyaona mabaya na kujificha;Bali wajinga huendelea mbele wakaumia.

13. Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni;Mtoza rehani aliye mdhamini wa malaya.

14. Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema;Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.

15. Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi,Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;

16. Atakaye kumzuia huyo huuzuia upepo;Na mkono wake wa kuume hukuta mafuta.

17. Chuma hunoa chuma;Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake.

18. Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;Naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.

19. Kama uso ufananavyo na uso katika maji;Kadhalika moyo wa mtu na mwenzake.

20. Kuzimu na Uharibifu havishibi;Wala macho ya wanadamu hayashibi.

21. Kalibu ni kwa fedha, na tanuru kwa dhahabu;Na mtu hujaribiwa kwa sifa zake.

22. Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni pamoja na ngano;Upumbavu wake hautamtoka.

23. Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako;Na kuwaangalia sana ng’ombe zako.

24. Kwa maana mali haziwi za milele;Na taji je! Yadumu tangu kizazi hata kizazi?

25. Manyasi huchukuliwa, na majani mabichi huonekana,Na maboga ya milimani hukusanyika.

Mit. 27