Mit. 27:1-11 Swahili Union Version (SUV)

1. Usijisifu kwa ajili ya kesho;Kwa maana hujui yatakayozaliwa na siku moja.

2. Mwingine na akusifu wala si kinywa chako mwenyewe;Mtu mgeni wala si midomo yako wewe.

3. Jiwe ni zito, na mchanga hulemea;Lakini ghadhabu ya mpumbavu ni nzito kuliko hivi vyote viwili.

4. Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika;Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu.

5. Lawama ya wazi ni heri,Kuliko upendo uliositirika.

6. Jeraha utiwazo na rafiki ni amini;Bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.

7. Nafsi iliyoshiba hukinai sega la asali;Bali nafsi yenye njaa huona kila kitu kichungu kuwa kitamu.

8. Kama ndege aendaye huko na huko mbali na kitundu chake;Ndivyo alivyo mtu aendaye huko na huko mbali na mahali pake.

9. Marhamu na manukato huufurahisha moyo;Kadhalika utamu wa rafiki ya mtu utokao katika kusudi la moyo wake.

10. Usimwache rafiki yako mwenyewe, wala rafiki ya baba yako,Wala usiende nyumbani mwa ndugu yako siku ya msiba wako.Afadhali jirani aliye karibu kuliko ndugu aliye mbali.

11. Mwanangu, uwe na hekima na kunifurahisha moyo wangu;Ili nipate kumjibu anilaumuye.

Mit. 27