9. Kama mwiba uingiao katika mkono wa mlevi;Kadhalika mithali katika kinywa cha mpumbavu.
10. Fundi stadi hufanyiza vitu vyote;Bali amwajiriye mpumbavu ni kama awaajiriye watu wapitao.
11. Kama vile mbwa arudiavyo matapiko yake;Kadhalika mpumbavu afanya upumbavu tena.
12. Je! Wamwona mtu mwenye hekima machoni pake mwenyewe?Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.
13. Mtu mvivu husema, Simba yuko njiani,Simba yuko katika njia kuu.