23. Midomo ijipendekezayo pamoja na moyo mbayaNi kama kigae kilichofunikizwa taka za fedha.
24. Achukiaye huficha chuki kwa midomo yake;Naye huweka akiba ya hila moyoni mwake.
25. Anenapo maneno mazuri usimsadiki;Kwa maana ana machukizo saba moyoni mwake.
26. Ingawa chuki hufunikizwa kwa hila;Uovu wake utadhihirika mbele ya kusanyiko.
27. Achimbaye shimo atatumbukia mwenyewe;Naye abingirishaye jiwe litamrudia.