Mit. 26:23-27 Swahili Union Version (SUV)

23. Midomo ijipendekezayo pamoja na moyo mbayaNi kama kigae kilichofunikizwa taka za fedha.

24. Achukiaye huficha chuki kwa midomo yake;Naye huweka akiba ya hila moyoni mwake.

25. Anenapo maneno mazuri usimsadiki;Kwa maana ana machukizo saba moyoni mwake.

26. Ingawa chuki hufunikizwa kwa hila;Uovu wake utadhihirika mbele ya kusanyiko.

27. Achimbaye shimo atatumbukia mwenyewe;Naye abingirishaye jiwe litamrudia.

Mit. 26