Mit. 26:2-13 Swahili Union Version (SUV)

2. Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake,Na kama mbayuwayu katika kuruka kwake;Kadhalika laana isiyo na sababu haimpigi mtu.

3. Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda,Na fimbo kwa mgongo wa mpumbavu.

4. Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake;Usije ukafanana naye.

5. Umjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake;Asije akawa mwenye hekima machoni pake.

6. Apelekaye ujumbe kwa mkono wa mpumbavuHujikata miguu, na kunywa hasara.

7. Miguu yake achechemeaye huwa dhaifu;Kadhalika mithali katika kinywa cha mpumbavu.

8. Kama mfuko wa vito katika chungu ya mawe;Kadhalika mtu amheshimuye mpumbavu.

9. Kama mwiba uingiao katika mkono wa mlevi;Kadhalika mithali katika kinywa cha mpumbavu.

10. Fundi stadi hufanyiza vitu vyote;Bali amwajiriye mpumbavu ni kama awaajiriye watu wapitao.

11. Kama vile mbwa arudiavyo matapiko yake;Kadhalika mpumbavu afanya upumbavu tena.

12. Je! Wamwona mtu mwenye hekima machoni pake mwenyewe?Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.

13. Mtu mvivu husema, Simba yuko njiani,Simba yuko katika njia kuu.

Mit. 26