Mit. 26:13-16 Swahili Union Version (SUV)

13. Mtu mvivu husema, Simba yuko njiani,Simba yuko katika njia kuu.

14. Kama vile mlango ugeukavyo katika bawaba zake;Kadhalika mtu mvivu katika kitanda chake.

15. Mtu mvivu hutia mkono wake sahanini;Kwamchosha kuupeleka tena kinywani pake.

16. Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake,Kuliko watu saba wawezao kutoa sababu.

Mit. 26