11. Kama vile mbwa arudiavyo matapiko yake;Kadhalika mpumbavu afanya upumbavu tena.
12. Je! Wamwona mtu mwenye hekima machoni pake mwenyewe?Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.
13. Mtu mvivu husema, Simba yuko njiani,Simba yuko katika njia kuu.
14. Kama vile mlango ugeukavyo katika bawaba zake;Kadhalika mtu mvivu katika kitanda chake.
15. Mtu mvivu hutia mkono wake sahanini;Kwamchosha kuupeleka tena kinywani pake.
16. Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake,Kuliko watu saba wawezao kutoa sababu.
17. Mtu apitaye na kujisumbua kwa ugomvi usio wake;Ni kama mtu ashikaye mbwa kwa masikio yake.