9. Ujitetee na mwenzako peke yake;Bali usiifunue siri ya mtu mwingine;
10. Yeye asikiaye asije akakutukana;Na aibu yako isiondoke.
11. Neno linenwalo wakati wa kufaa,Ni kama machungwa katika vyano vya fedha.
12. Kipuli cha dhahabu, na pambo la dhahabu safi;Ndivyo alivyo mwonyaji mwenye hekima kwa sikio lisikialo.
13. Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno;Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwao wamtumao;Kwa maana huwaburudisha bwana zake nafsi zao.