6. Usijitukuze mbele ya uso wa mfalme;Wala usisimame mahali pa watu wakuu;
7. Kwa maana ni heri kuambiwa, Njoo huku mbele;Kuliko kuwekwa nyuma machoni pa mkuu.Yale uliyoyaona kwa macho,
8. Usitoke nje kwa haraka ili kuyashindania;Usije ukakosa kujua la kutenda hatimaye,Mwenzako atakapokuwa amekuaibisha.
9. Ujitetee na mwenzako peke yake;Bali usiifunue siri ya mtu mwingine;
10. Yeye asikiaye asije akakutukana;Na aibu yako isiondoke.
11. Neno linenwalo wakati wa kufaa,Ni kama machungwa katika vyano vya fedha.