13. Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno;Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwao wamtumao;Kwa maana huwaburudisha bwana zake nafsi zao.
14. Kama mawingu na upepo pasipo mvua;Ndivyo alivyo yeye ajisifiaye karama kwa uongo.
15. Kwa uvumilivu mwingi mkuu husadikishwa;Na ulimi laini huvunja mfupa.
16. Je! Umeona asali? Kula kadiri ya kukutosha;Usije ukashiba na kuitapika.