Mit. 25:13-16 Swahili Union Version (SUV)

13. Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno;Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwao wamtumao;Kwa maana huwaburudisha bwana zake nafsi zao.

14. Kama mawingu na upepo pasipo mvua;Ndivyo alivyo yeye ajisifiaye karama kwa uongo.

15. Kwa uvumilivu mwingi mkuu husadikishwa;Na ulimi laini huvunja mfupa.

16. Je! Umeona asali? Kula kadiri ya kukutosha;Usije ukashiba na kuitapika.

Mit. 25