Mit. 24:4-14 Swahili Union Version (SUV)

4. Na kwa maarifa vyumba vyake hujazwaVitu vyote vya thamani na vya kupendeza.

5. Mtu mwenye hekima ana nguvu;Naam, mtu wa maarifa huongeza uwezo;

6. Maana kwa mashauri ya akili utafanya vita;Na kwa wingi wa washauri huja wokovu.

7. Kwa mpumbavu hekima haipatikani;Hafumbui kinywa chake langoni.

8. Mtu afikiriye kutenda maovu,Watu watamwita mtundu;

9. Fikira za mpumbavu ni dhambi,Na mwenye mzaha huwachukiza watu.

10. Ukizimia siku ya taabu,Nguvu zako ni chache.

11. Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe;Nao walio tayari kuchinjwa uwaopoe.

12. Ukisema, Sisi hatukujua hayo;Je! Yeye aipimaye mioyo siye afahamuye?Naye ailindaye nafsi yako siye ajuaye?Je! Hatamlipa kila mtu sawasawa na kazi yake?

13. Mwanangu, ule asali, kwa maana ni njema,Na sega la asali lililo tamu ulionjapo.

14. Basi utaijua hekima kuwa tamu kwa nafsi yako;Ikiwa umekwisha kuiona;Ndipo itakapofuata thawabu;Wala tumaini lako halitabatilika.

Mit. 24