Mit. 24:4-10 Swahili Union Version (SUV)

4. Na kwa maarifa vyumba vyake hujazwaVitu vyote vya thamani na vya kupendeza.

5. Mtu mwenye hekima ana nguvu;Naam, mtu wa maarifa huongeza uwezo;

6. Maana kwa mashauri ya akili utafanya vita;Na kwa wingi wa washauri huja wokovu.

7. Kwa mpumbavu hekima haipatikani;Hafumbui kinywa chake langoni.

8. Mtu afikiriye kutenda maovu,Watu watamwita mtundu;

9. Fikira za mpumbavu ni dhambi,Na mwenye mzaha huwachukiza watu.

10. Ukizimia siku ya taabu,Nguvu zako ni chache.

Mit. 24