Mit. 24:28-33 Swahili Union Version (SUV)

28. Usimshuhudie jirani yako pasipo sababu,Wala usidanganye kwa midomo yako.

29. Usiseme, Nitamtenda kama alivyonitenda mimi;Nitamlipa mtu huyo sawasawa na tendo lake.

30. Nalipita karibu na shamba la mvivu,Na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili.

31. Kumbe! Lote pia limemea miiba;Uso wake ulifunikwa kwa viwawi;Na ukuta wake wa mawe umebomoka.

32. Ndipo nilipoangalia na kufikiri sana;Naliona, nikapata mafundisho.

33. Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,Bado kukunja mikono upate usingizi!

Mit. 24