Mit. 24:26-33 Swahili Union Version (SUV)

26. Aibusu midomo atoaye jawabu la haki.

27. Tengeneza kazi yako huko nje,Jifanyizie kazi yako tayari shambani,Ukiisha, jenga nyumba yako.

28. Usimshuhudie jirani yako pasipo sababu,Wala usidanganye kwa midomo yako.

29. Usiseme, Nitamtenda kama alivyonitenda mimi;Nitamlipa mtu huyo sawasawa na tendo lake.

30. Nalipita karibu na shamba la mvivu,Na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili.

31. Kumbe! Lote pia limemea miiba;Uso wake ulifunikwa kwa viwawi;Na ukuta wake wa mawe umebomoka.

32. Ndipo nilipoangalia na kufikiri sana;Naliona, nikapata mafundisho.

33. Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,Bado kukunja mikono upate usingizi!

Mit. 24