Mit. 24:23-27 Swahili Union Version (SUV)

23. Haya nayo pia ni maneno ya wenye akili.Kupendelea watu katika hukumu si kwema.

24. Amwambiaye mtu mwovu, Wewe una haki;Kabila za watu watamlaani, taifa watamchukia.

25. Bali kwao wakemeao furaha itakuwako;Na baraka ya kufanikiwa itawajilia.

26. Aibusu midomo atoaye jawabu la haki.

27. Tengeneza kazi yako huko nje,Jifanyizie kazi yako tayari shambani,Ukiisha, jenga nyumba yako.

Mit. 24