23. Haya nayo pia ni maneno ya wenye akili.Kupendelea watu katika hukumu si kwema.
24. Amwambiaye mtu mwovu, Wewe una haki;Kabila za watu watamlaani, taifa watamchukia.
25. Bali kwao wakemeao furaha itakuwako;Na baraka ya kufanikiwa itawajilia.
26. Aibusu midomo atoaye jawabu la haki.
27. Tengeneza kazi yako huko nje,Jifanyizie kazi yako tayari shambani,Ukiisha, jenga nyumba yako.